Aveva amrudisha kundini Dewji

Makamu Mwenyekiti Kamati ya Usajili, Kassim Dewji.

Muktasari:

Pia Aveva amemteua Hans Pope kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili akisaidiwa na Kassim Dewji, huku wajumbe wakiwa Said Tully, Mulamu Nghambi na Rodney Chiduo.

Dar es Salaam. Rais mpya wa Simba, Evans Aveva ameteua wajumbe wa kuunda Kamati ya Utendaji ya klabu hiyo.

Wajumbe hao ni Mohamed Nassoro ‘Kigoma’, Musley Ruwei na Salim Abdallah ‘Try Again’.

Pia Aveva amemteua Hans Pope kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili akisaidiwa na Kassim Dewji, huku wajumbe wakiwa Said Tully, Mulamu Nghambi na Rodney Chiduo.

Kamati ya Mashindano itaongozwa na Kigoma akisaidiana na Geofrey Nyange, huku wajumbe wakiwa Mohamed Mlanzi ‘Meddy’, Hussein Simba na Idd Kajuna.