Kagera yarudishiwa pointi tatu

Muktasari:

Akitangaza uamuzi huo Katibu Mkuu wa TFF, Selestine Mwesigwa amesema Kamati ya sheria imebaini mapungufu kadhaa katika maamuzi ya Kamati ya saa 72 kwa kwanza rufaa ya Simba kukatwa nje ya wakati lakini pia haikulipiwa ada ya sh 300000.

Kamati ya sheria na hadhi za wachezaji imebatilisha uamuzi ya Kamati ya saa 72 kwa kuipa simba pointi tatu na kuzirudisha Kagera Sugar.
Akitangaza uamuzi huo Katibu Mkuu wa TFF, Selestine Mwesigwa amesema Kamati ya sheria imebaini mapungufu kadhaa katika maamuzi ya Kamati ya saa 72 kwa kwanza rufaa ya Simba kukatwa nje ya wakati lakini pia haikulipiwa ada ya sh 300000.
Mbali na hivyo Mwesigwa amesema Kamati ya saa 72 ilipokutana iliruhusu watu wasiokuwa wajumbe wa Kamati kushiriki kufanya uamuzi kitu ambacho ni kosa.
Mbali na uamuzi huo Kamati imeitaka TFF kuwachukulia hatua baadhi ya watendaji wa bodi kwa kuipotosha Kamati ya saa 72