Kichuya mchezaji bora wa mwezi

Mshambuliaji wa Simba, Shiza Kichuya

Muktasari:

Kichuya aliwashinda wachezaji Adam Kingwande wa Stand United na Omari Mponda wa Ndanda FC.

Dar es Salaam. Mshambuliaji wa Simba, Shiza Kichuya amechaguliwa kuwa Mchezaji Bora wa Ligi Kuu ya Vodacom kwa Septemba msimu wa 2016/2017.
Kichuya aliwashinda wachezaji Adam Kingwande wa Stand United na Omari Mponda wa Ndanda FC.
Kichuya aliisadia timu yake kwa mwezi huo kupata pointi zote 12 katika mechi nne ilizocheza, matokeo ambayo yameifanya Simba iendelee kuongoza Ligi hiyo inayoshirikisha timu 16. Pia alifunga mabao matatu katika mechi mbili kati ya nne ilizocheza timu yake.
Kwa kushinda tuzo hizo ya mwezi, Kichuya atazawadiwa kitita cha Sh. 1milioni kutoka kwa wadhamini wa Ligi hiyo, kampuni ya Vodacom Tanzania.