Mshambuliaji Mjapani wa Arsenal akosa kibali cha kucheza soka England

Muktasari:

Mshambuliaji huyo Mjapani (21), alitua Arsenal akitokea Sanf Hiroshima mwaka jana bado ameshindwa kuwa na vigezo vya kupata kibali cha kufanya kazi ndani ya England.

Arsenal haitakuwa na huduma ya mshambuliaji wake Takuma Asano kwa msimu ujao na ataendelea kucheza kwa mkopo huko Stuttgart baada ya kushindwa kupata kibali cha kupata kali England.

Mshambuliaji huyo Mjapani (21), alitua Arsenal akitokea Sanf Hiroshima mwaka jana bado ameshindwa kuwa na vigezo vya kupata kibali cha kufanya kazi ndani ya England.

Jambo linamewafanya mashabiki wa Arsenal kuendelea tu kuisubiri huduma ya mshambuliaji huyo pengine hadi mwakani.