Richardson afikisha idadi ya makipa saba Manchester United

London, England. Kocha Jose Mourinho amemsajili kipa Theo Richardson (18) atakayempa ushindani David De Gea msimu huu.

Usajili wa kipa huyo mpya umefikisha idadi ya makipa saba kwenye klabu ya Manchester United ambao ni De Gea, Romero, Joel Pereira, Kieran O’Hara, Max Johnstone, Ilias Moutha-Sebtaoui.

Taarifa iliyotolea jana kipa huyo amesajiliwa kwa mkataba wa kudumu ambapo ataanza kuonyesha makali yake msimu huu mpya Ligi Kuu England utakapoanza.

Kipa huyo aliyechukuliwa kutoka timu ya vijana ya Leeds United  hivi karibuni alikuwa kwenye mechi za majaribio na Manchester United.