Wabunge mashabiki wa Simba chali
Muktasari:
Mabao ya Mwigulu Nchemba, Hamis Sadifa, Ridhiwani Kikwete na Mohammed Mchengerwa yametosha kuwapa furaha mashabiki na wapenzi wa Yanga na ushindi dhidi ya wapinzani wao, Simba.
Dar es Salaam. Wabunge wanaoshabikia Yanga wameibuka na ushindi wa mabao 5-2 dhidi ya watani zao, Simba.
Mabao ya Mwigulu Nchemba, Hamis Sadifa, Ridhiwani Kikwete na Mohammed Mchengerwa yametosha kuwapa furaha mashabiki na wapenzi wa Yanga na ushindi dhidi ya wapinzani wao, Simba.
Mechi hii ni maalumu kwa ajili ya kuchangia waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera na imechezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.