Yanga, Simba na Azam kikwazo Stars

Muktasari:

Taifa Stars imepangwa Kundi L na timu za Uganda, Cape Verde na Lesotho katika harakati za kuwania kucheza mashindano ya Afcon 2019 na michezo yake itaanza Juni 5 mwaka huu.

Dar es Salaam.Licha ya Tanzania kuwa na mikakati  ya kuhakikisha timu ya Taifa ‘Taifa Stars’ inafuzu kucheza fainali za Mataifa Afrika 2019 zitakazofanyika Cameroon, mikakati hiyo ya kiufundi haiendi sambamba na ile inayotekelezwa na makocha wa klabu za Ligi Kuu.

Taifa Stars imepangwa Kundi L na timu za Uganda, Cape Verde na Lesotho katika harakati za kuwania kucheza mashindano ya Afcon 2019 na michezo yake itaanza Juni 5 mwaka huu.

Mathalani, Simba, Yanga na Azam ambazo zinatoa wachezaji wengi kwenye kikosi cha timu ya Taifa Taifa Stars, lakini kwa sasa hawapati nafasi ya kucheza kwenye timu zao.