Waziri aanza harakati za kufufua utalii kusini

Muktasari:

  • Waziri Kigwangalla ametoa  mfano mwaka 2008 hadi 2009 ambapo kulitokea  mdororo wa  uchumi duniani Kenya iliadhirika zaidi ya Tanzania kutokana na vivutio walivyonavyo lakini hivi sasa iko mbele zaidi ya Tanzania amesema

Waziri wa Maliasili na Utalii Dk Khamis Kigwangalla  amesema Kanda ya Kaskazini imeelemewa kutokana na idadi kubwa ya watalii.

Dk Kigwangalla  amesema  hayo leo  katika kikao cha mawaziri wa wizara hiyo na wadau wa sekta ya maliasili na utalii alichokiitisha yeye mwenyewe.

Amesema kwamba kutokana na kanda hiyo kuelemewa  wameanza kufufua utalii katika kanda nyingine ikiwemo kusini.

Dk Kigwangalla akiwa  ameongozana na Naibu wake Japhet Hasunga, amesema  sekta ya maliasili inaingiza mapato mengi kwa taifa lakini ikifanyiwa kazi inaweza kuongeza mapato zaidi.

"Pamoja na sifa zote bado tunahitaji kuongeza nguvu ili kuongeza tija zaidi kwa Taifa," amesema

Amesema  kuna mifano ya nchi ambazo zimejizatiti katika utalii tu na zinajiendesha.

.

 Amesema  kuna kazi  kubwa ya kufanya na kwamba baadhi ya vyombo vya habari na mitandao ya jamii wameandika kuhusu wizara hiyo ilivyopitiwa na mawaziri wengi na hivyo ameamua kuwasikiliza wadau hao kabla ya kubeba mzigo huo mzito.

Amesema  wengine wanasema  wizara hiyo ni geti la kutokea na kuongeza kuwa zipo changamoto katika sheria zetu, tozo na nimepokea  maoni ni mengi sana kutoka kwa wadau.

 Amesema  kuna mambo yangeweza kushughulikiwa ambayo yanatakiwa kuwa katika sheria moja na zinahitaji

kufanya sheria zisikinzane.

Amesema  changamoto nyingine ni ubora mdogo wa huduma mbalimbali kwa watalii kuanzia uwanja wa ndege hadi anapofika kwenye vivutio.