Minyoo, matende, kichocho ni hatari

Muktasari:

Vilevile watu milioni 12.5 wapo  hatarini kupata ugonjwa wa Trakoma huku milioni 4 wakiwa hatarini kupata ugonjwa wa usubi.

Dar es Salaam. Watu milioni 47  nchini  wapo katika hatari ya kupata magonjwa  ambayo yalikuwa hayapewi kipaumbele yakiwemo  Minyoo,Matende na Kichocho.

Vilevile watu milioni 12.5 wapo  hatarini kupata ugonjwa wa Trakoma huku milioni 4 wakiwa hatarini kupata ugonjwa wa usubi.

Hayo yamebainishwa jijini Dar es Salaam leo na ofisa mpango wa kudhibiti magonjwa ambayo yalikuwa hayapewi kipaumbele, Oscar Kaitaba  kutoka Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, wakati  akitoa  mafunzo   kwa  waandishi wa habari juu  ya  mpango wa Taifa wa kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele.

Kaitaba amesema  katika  wagonjwa   milioni 47 waliopo hatarini kupata matende, kichocho na minyoo,  watu ambao wapo  hatarini kupata ugonjwa  wa  minyoo  ni wale  ambao wanakula chakula ambacho hakijaiva.