Mkapa kuhudhuria kuapishwa Kagame

Rais mstaafu wa Tanzania, Benjamin Mkapa 

Muktasari:

Mkapa ambaye ujumbe wake uko nchini Burundi kwa ajili ya mazungumzo na Serikali ya nchi hiyo katika jitihada za kusuluhisha mzozo wa kisiasa aliwasili jana mjini Kigali akiwa miongoni mwa viongozi zaidi 20 ambao wanahudhuria sherehe hizo.

Dar es Salaam. Rais mstaafu wa Tanzania, Benjamin Mkapa ni miongoni mwa viongozi mbalimbali wa Afrika wanaohudhuria sherehe za kuapishwa kwa Rais wa Rwanda, Paul Kagame aliyeshinda katika uchaguzi uliofanyika Agosti 4.

Mkapa ambaye ujumbe wake uko nchini Burundi kwa ajili ya mazungumzo na Serikali ya nchi hiyo katika jitihada za kusuluhisha mzozo wa kisiasa aliwasili jana mjini Kigali akiwa miongoni mwa viongozi zaidi 20 ambao wanahudhuria sherehe hizo.

Sherehe hizo ambazo zinatarajiwa kupambwa na burudani mbalimbali zinafanyika katika Uwanja wa Taifa wa Amahoro. Rais Kagame atakuwa anaanza muhula wa kwanza wa miaka saba tangu taifa hilo lilipofanyia marekebisho katiba yake.

Miongoni mwa viongozi wa Afrika wanaohudhuria sherehe hizo ni pamoja na Rais wa Jamhuri ya Afrika ya Kati, Faustin-Archange Touadera ambaye alikuwa wa kwanza kuwasili nchini humo.

Wengine ni Rais wa Kenya, Uhuru Kenya,  Rais wa Djibouti, Ismail Omar Guelleh, Rais wa  Niger, Mahamadou Issoufou, Rais wa Senegal, Macky Sally, Rais wa Zambia, Edgar Lungu na Rais wa Congo Brazaville,  Sassou Nguesso