Mnorway aipigia chapuo gesi mpya

Muktasari:

Gesi ya helium ambayo ni adimu hutumiwa kwenye vifaa vya kitabibu kama mashine ya kuchukulia vipimo vya MRI Scanner, kubashiri moto viwandani, kuunganisha vyuma na nishati ya nyuklia.

Dar es Salaam. Ofisa Mtendaji Mkuu wa kampuni yenye mradi wa nishati hiyo nchini Norway, Thomas Abraham-James amesema  Tanzania inaweza kuingiza fedha nyingi za kigeni kutokana na kugunduliwa kwa gesi adimu ya helium.
“Gesi ya helium ina biashara kubwa katika soko la kimataifa,  lakini ukosekanaji wa soko unatokana na bidhaa hiyo kuwa adimu hivyo huenda Tanzania ikasaidia kuongeza soko la gesi ya helium katika soko la kimataifa pale itakapoanza kuzalishwa na kuuzwa nje ya nchi," amesema.
Gesi ya helium ambayo ni adimu hutumiwa kwenye vifaa vya kitabibu kama mashine ya kuchukulia vipimo vya MRI Scanner, kubashiri moto viwandani, kuunganisha vyuma na nishati ya nyuklia.
Gesi hiyo pia hutumika kubaini alama kwenye za utambulisho wa bidhaa. Kwa Tanzania gesi ya helium iligunduliwa na wataalamu kutoka Uingereza Juni mwishoni mwaka huu.