Mshtakiwa wa Sh7 milioni kwa dakika ndani ya kesi mpya

Muktasari:

Mshtakiwa wa kwanza katika kesi ya uhujumu uchumi, anayedaiwa kuiibia Serikali na kuisababishia hasara ya zaidi ya Sh15.6 kwa kutumia mashine za kodi za kielektroniki, Mohamde Yusufali, anatarajiwa kupandishwa kizimbani na kusomewa mashtaka mengine ya uhujumu uchumi.

Dar es Salaam. Mshtakiwa wa kwanza katika kesi ya uhujumu uchumi, anayedaiwa kuiibia Serikali na kuisababishia hasara ya zaidi ya Sh15.6 bilioni kwa kutumia mashine za kodi za kielektroniki, Mohamde Yusufali, anatarajiwa kupandishwa kizimbani na kusomewa mashtaka mengine ya uhujumu uchumi.

Katika kesi hiyo, Yusufali anatarajiwa kuunganishwa na mfanyabiashara maarufu jijini Arusha, aliyetajwa kwa jina la Samweli Lema, ambao watasomewa mashtaka yanayowakabili katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam.

Yusufali na Lema walifikishwa mahakamani hapo jana alasiri na Takukuru ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru),kwa lengo la kupandishwa kizimbani na kusomewa mashtaka yanayowakabili.