Mtatiro ahoji mamlaka ya Msigwa Ikulu

Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya CUF, upande wa Katibu Mkuu wa  CUF, Maalim Seif Sharif, Julius Mtatiro

Muktasari:

Wajumbe hao wapya watashiriki kikao cha NEC kitakachofanyika wiki ijayo.


Dar es Salaam. Rais John Magufuli amemteua Waziri Mkuu wa zamani, Mizengo Pinda na Makongoro Nyerere kuwa Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa, CCM (NEC).

 Hata hivyo taarifa hiyo  iliyotumwa  saa nane usiku wa kuamkia leo Mei 25, na Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Gerson Msigwa ilizua mjadala kwa baadhi ya wanasiasa na wadau wa masuala ya siasa kuhoji mamlaka ya Msemaji wa Ikulu na yale ya Ofisi ya Itikadi na Uenezi ya CCM.

 Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya CUF, upande wa Katibu Mkuu wa chama hicho, Maalim Seif Sharif, Julius Mtatiro, amesema kitendo cha Msemaji wa Ikulu (Mtumishi wa Serikali) kutangaza vikao vya CCM na uteuzi wa wajumbe wa vikao vya CCM ni hatari.

“Watanzania wanalazimishwa kukubali kuwa watumishi wa Serikali ni watumishi wa CCM. CCM ina msemaji wake lakini mambo ya CCM yanatangazwa na Ikulu.” amesema