Mvua yaua mwanafunzi Kibohehe

Muktasari:

Mvua hiyo iliyoandamana na upepo mkali iliangusha ukuta wa chumba cha darasa.

 

 Mwanafunzi mmoja wa darasa la sita wa Shule ya Msingi

Kibohehe, iliyoko wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro, amefariki dunia na

wengine watano kujeruhiwa, baada ya kuangukiwa na ukuta.

Mwanafunzi huyo wa kiume ameangukiwa na ukuta wa chumba cha

darasa baada ya mvua kubwa iliyoambatana na upepo kunyesha leo

mchana.

Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya Simu, Kamanda wa Polisi Mkoa wa

Kilimanjaro, Hamis Issah, amesema mwanafunzi huyo alikuwa akiingia

kwenye kipindi cha dini na ndipo alipokutana na ajali hiyo ya ukuta na

kupoteza maisha

“Mvua ilinyesha na upepo mkali, jengo moja la darasa likadondoka na

kumwangukia mtoto huyo ambaye alikuwa akiingia kwenye kipindi cha

dini,”amesema Issah.

Aidha Kamanda amesema, majeruhi wamepelekwa katika Hospitali ya Wilaya

ya Hai kwa ajili ya matibabu na kwamba uchunguzi zaidi wa tukio hilo

bado unaendelea.