Mvutano wamachinga, mgambo waibuka tena Mwanza
Mwanza. Umeibuka upya mvutano baina ya mgambo wa jiji la Mwanza na wamachinga baada ya kutakiwa kuondoka eneo la Makoroboi katikati ya msikiti wa Swaminarayan.
Kutokana na vurugu hizo kwa sasa barabara inayounganisha kituo mabasi cha zamani cha Tanganyika imefungwa kukiwa na ulinzi mkali wa mgambo na polisi wa FFU.