Mvutano wamachinga, mgambo waibuka tena Mwanza

Baadhi ya askari na mgambo wa jiji wakiwa wameimarisha ulinzi katika eneo hilo la makoroboi kwenye msikiti wa Swinarayan jijini Mwanza

Mwanza. Umeibuka upya mvutano baina ya  mgambo wa jiji la Mwanza na wamachinga baada ya kutakiwa kuondoka eneo la Makoroboi katikati ya msikiti wa Swaminarayan.

Kutokana na vurugu hizo kwa sasa barabara inayounganisha kituo mabasi cha zamani cha Tanganyika imefungwa kukiwa na ulinzi mkali wa mgambo na polisi wa FFU.