Mwanafunzi wa kitanzania ashinda insha Umoja wa Mataifa

Mwanafunzi wa  Kitanzania, Amani Alfred Naburi

Muktasari:

Naburi ni  Mtanzania  anayesoma   Chuo Kikuu cha  African Leadership,  huko Mauritius na walitakiwa kuandika   kwa  lugha sita zinazotumika na Umoja wa Mataifa. Lugha hizo ni  Kiingereza, Kifaransa,  Kiarabu, Kichina, Kispanishi na  Kirusi

Mwanafunzi wa  Kitanzania, Amani Alfred Naburi,   ni mmoja wa  kati ya  wanafunzi 60 kutoka     Vyuo  Vikuu mbalimbali  duniani ambao wameshinda shindano la  Insha   lijulikanayo kama   “Lugha nyingi, Dunia Moja” ( Many  languages, One World) lililoandaliwa kwa ushirikiano baina ya  United Nations Academic Impact ( UNAI) na ELS Educational Services, Inc.

Naburi ni  Mtanzania  anayesoma   Chuo Kikuu cha  African Leadership,  huko Mauritius na walitakiwa kuandika   kwa  lugha sita zinazotumika na Umoja wa Mataifa. Lugha hizo ni  Kiingereza, Kifaransa,  Kiarabu, Kichina, Kispanishi na  Kirusi

Washindani wa Insha hiyo  walitakiwa kuandisha Insha  juu ya namna watakavyochangia katika utekelezaji  wa  Malengo  Mapya ya Maendeleo Endelevu ( Agenda (2030). Ambapo  kila moja wapo alitakiwa kuiandika insha  hiyo   yenye  maneno yasiyozidi 2,000 kwa  lugha  nje ya lugha yake ya   asili ya nchi anayotoka.