Ngeleja ampa siku tatu DED

Mbunge wa Sengerema William Ngeleja

Muktasari:

Hata hivyo, Kaimu Mkurugenzi huyo amesema hajagawa madawati yaliyotokana na fedha za mfuko wa jimbo bali anagawa madawati yaliyopo katika karakana.

Sengerema. Mbunge wa Sengerema William Ngeleja ametoa siku tatu kurejeshewa madawati yaliyotengenezwa kwa fedha za mfuko wa jimbo

Agizo hilo amelitoa kwa Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema Visent Bushaija kutokana na madawati hayo kusambazwa shuleni bila kukaguliwa na kuwekewa nembo.

Hata hivyo, Kaimu Mkurugenzi huyo amesema hajagawa madawati yaliyotokana na fedha za mfuko wa jimbo bali anagawa madawati yaliyopo katika karakana.

“Hakuna dawati hata moja lililotoka kwenda shuleni, madawati yanayotoka kwenda shuleni ni yale yanayotokana na wahisani mbalimbali pamoja na fedha za halmashauri pekee,”amesema.