Dk Tulia, Waziri Mwakyembe kumnadi Mwinuka

Muktasari:

  • Wengine waliojitokeza katika viwanja Mwaikambo mjini Kyela jijini Mbeya ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC), Dk Steven Mwakajumilo na viongozi wengine wa CCM jijini humo.

Mbeya. Naibu Spika, Dk Tulia Ackson na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe wamejitokeza kuzindua kampeni za mgombea udiwani Mwanganyanga, Alex  Mwinuka.

Wengine waliojitokeza katika viwanja Mwaikambo mjini Kyela jijini Mbeya ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC), Dk Steven Mwakajumilo na viongozi wengine wa CCM jijini humo.

CCM inafanya uzinduzi wake rasmi katika kampeni za uchaguzi huo wa marudio, baada ya aliyekuwa diwani wa kata hiyo, Wilson Mwalyaje (Chadema) kufariki dunia Februari mwaka huu.