Pato halisi la Taifa limeongezeka kwa zaidi ya Sh3 trilioni
Muktasari:
Waziri amesema pato la kila mwananchi limeongezeka kutoka Sh 2.1 milioni mwaka 2016 mpaka Sh 2.3 kwa mwaka.
Dodoma. Serikali imesema Pato Halisi la Taifa limeongezeka kutoka Sh47.1 mwaka 2016 trilioni mpaka Sh50.5 trilioni mwaka jana.
Hayo yamesemwa leo Juni 13 na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango alipokuwa akieleza mwenendo wa uchumi kwa mwaka 2017.
"Sekta zilizochangia kuimarika kwa pato hilo ni uchimbaji madini na mawe iliyokua kwa asilimia 17.5, uchukuzi na usafirishaji mizigo asilimia 16.6 na habari na mawasiliano asilimia 14.7," amesema Waziri Mpango.
Kutokana na kuimarika kwa pato la taifa, waziri alisema hata pato la mtu mmoja mmoja nalo likiimarika.
Waziri amesema pato la kila mwananchi limeongezeka kutoka Sh 2.1 milioni mwaka 2016 mpaka Sh 2.3 kwa mwaka.