VIDEO: Polisi: Tunafuatilia tukio la kutekwa Mo Dewji

Mfanyabiashara Mohammed Dewji

Muktasari:

  • Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema wanafuatilia taarifa za madai ya kutekwa mfanyabiashara Mohammed Dewji.

Dar es Salaam. Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema polisi wanafuatilia taarifa za madai ya kutekwa kwa mfanyabiashara, Mohammed Dewji.

Akizungumza na MCL Digital leo asubuhi Oktoba 11, 2018 Mambosasa amesema baada ya kupata taarifa za tukio hilo wanafuatilia kujua ukweli wake.

Taarifa zilizoifikia MCL Digital leo asubuhi zinaeleza kuwa mfanyabiashara huyu anadaiwa kutekwa leo asubuhi maeneo ya hoteli ya Collessium jijini Dar es Salaam.

Dewji ni mwekezaji wa klabu ya Simba akiwa na hisa 49 na amekuwa akiingia katika chati ya juu ya jarida la Forbes kama miongoni mwa matajiri vijana Afrika.

Endelea kufuatilia MCL Digital kwa taarifa zaidi