Babu Seya, Papi Kocha waachiwa huru

Muktasari:

Wameachiwa huru baada ya kukaa jela tangu 2004

Dar es Salaam. Rais John Magufuli   leo Jumamosi ametoa msamaha mwanamuziki Nguza Viking pamoja mtoto wake  wake  Papi Kocha waliokuwa wakitumikia kifungo cha maisha kwa makosa ya kuwanajisi watoto.

Rais Magufuli ametoa msamaha huo wakati akihutubia maadhimisho ya shehere za Uhuru wa Tanzania Bara yaliyofanyika mjini Dodoma leo.

Familia hiyo imekaa jela tangu ilipohukumiwa adhabu hiyo Juni 5, 2004.