Babu Seya, Papi Kocha waachiwa huru
Muktasari:
Wameachiwa huru baada ya kukaa jela tangu 2004
Dar es Salaam. Rais John Magufuli leo Jumamosi ametoa msamaha mwanamuziki Nguza Viking pamoja mtoto wake wake Papi Kocha waliokuwa wakitumikia kifungo cha maisha kwa makosa ya kuwanajisi watoto.
Rais Magufuli ametoa msamaha huo wakati akihutubia maadhimisho ya shehere za Uhuru wa Tanzania Bara yaliyofanyika mjini Dodoma leo.
Familia hiyo imekaa jela tangu ilipohukumiwa adhabu hiyo Juni 5, 2004.