Rais Magufuli amwondoa IGP Mangu, Simon Sirro amrithi

Muktasari:

Taarifa iliyotolewa na Ikumu muda mfupi uliopita inasema aliyekuwa IGP, Ernest Mangu, atapangiwa kazi nyingine.

Dar es Salaam. Rais John Magufuli amemteua Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Simon Sirro, kuwa Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP).

Taarifa iliyotolewa na Ikumu muda mfupi uliopita inasema aliyekuwa IGP, Ernest Mangu, atapangiwa kazi nyingine.

Taarifa iliyotolewa na katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi, inaeleza kuwa Sirro ataapishwa kesho Jumatatu ya Mei 29, 2017 saa 3.00 asubuhi Ikulu jijini Dar es Salaam.