Serengeti Boys yafuzu Afcon U-17

Muktasari:

Serengeti Boys ilifuzu baada ya kushinda rufaa yake dhidi ya Congo iliyomchezesha mchezaji aliyezidi umri.

Dar es Salaam. Tanzania imefuzu kwa mara ya kwanza kucheza fainali za Mataifa ya Afrika kwa vijana U-17 zitakazofanyika Gabon mwaka huu.

Serengeti Boys ilifuzu baada ya kushinda rufaa yake dhidi ya Congo iliyomchezesha mchezaji aliyezidi umri.

Tanzania itaingia Kundi B ikichukua nafasi ya Congo kundi hilo lina timu za Niger, mabingwa watetezi Mali na Angola.

Timu nne zinazofanikiwa kuingia katika nusu fainali zitafuzu moja kwa moja  Kombe la Dunia la Fifa U17 litalofanyika India baadaye mwaka huu.

Waziri wa Michezo, Nape Nnauye aliandika kwenye akaunti yake ya twiter kuipongeza Serengeti Boys kwa kufikia hatua hiyo.

“Mungu Mkubwa! Tumefuzu kwenye fainali za Afrika chini ya umri wa miaka 17. Nia, uwezo na sababu za kuchukua kombe hili tunazo. Hongera TZ” aliandika Nape.