Serikali yaongeza ushuru wa pipi, chokoleti

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, mawaziri na wabunge wakifatilia hotuba ya Bajeti Kuu ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2018/2019 kwa kusoma na wengine kumsikiliza Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango alipokuwa akiwasilisha bungeni, jijini Dodoma leo. Picha na Edwin Mjwahuzi

Muktasari:

Waziri Mpango amesema nchi za Afrika Mashariki zina uwezo wa kuzalisha chokoleti na kutosheleza mahitaji ya soko.


Dodoma. Ili kuhamasisha uzalishaji wa ndani, Serikali imetangaza kupandisha ushuru wa forodha kwenye peremende, chokoleti, bazoka (chewing corn) na nyanya zilizosindikwa kutoka nje.

Akizungumza bungeni leo Juni 14, wakati akiwasilisha bajeti kuu ya serikali kwa mwaka wa fedha 2018/19, Dk Mpango amesema ushuru huo umeongezeka kwa asilimia 10 kutoka asilimia 25 iliyokuwa inatozwa mwaka huu wa fedha mpaka asilimia 35 kuanzia Julai Mosi.

“Lengo la hatua hii ni kulinda uzalishaji wa bidhaa hizo katika viwanda vya ndani, ajira,” amesema Dk Mpango.

Waziri Mpango amesema nchi za Afrika Mashariki zina uwezo wa kuzalisha  chokoleti na kutosheleza mahitaji ya soko.