Shule nyingine yaungua Arusha

Arusha. Ikiwa takribani wiki ipite tangia Shule ya sekondari Lowasa kuungua, moto umezuka tena na kuteketeza mabweni ya Shule ya Sekondari Mlangarini

Shule hiyo iliyopo Wilaya ya Arumeru, jijini Arusha imekuwa ni miongoni mwa shule 5 ambazo ndani ya mwezi moja zimeteketea kwa moto huku uchunguzi bado ukiwa bado unaendelea

Kufuatia kuwaka kwa moto na kuteketeza sehemu kubwa ya bweni la wavulana watu wanne wanashikiliwa na jeshi la polisi kwa mahojiano.

Akitaja waliokamatwa mkuu wa shule hiyo Elias Johhn Pallakyo alisema ni  walinzi wawili pamoja na walimu wawili wa zamu kwa usiku huo