Sita wafutiwa adhabu ya kunyongwa hadi kufa

Muktasari:

Uamuzi huo ulisomwa jana na Jaji Projest Rugazia wa Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam baada ya kutolewa na jopo la majaji watatu wa Mahakama ya Rufani lililoongozwa na Jaji Mkuu, Mohamed Chande. Wengine ni Jaji Ibrahimu Juma na Jaji Augustine Mwarija.

Dar es Salaam. Mahakama ya Rufani imewafutia adhabu ya kunyongwa hadi kufa na kuamuru kuachiwa huru watu sita waliohukumiwa kwa mauaji  ya askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) na mfanyakazi wa Benki ya NMB, tawi la Wami Morogoro.

Uamuzi huo ulisomwa jana na Jaji Projest Rugazia wa Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam baada ya kutolewa na jopo la majaji watatu wa Mahakama ya Rufani lililoongozwa na Jaji Mkuu, Mohamed Chande. Wengine ni Jaji Ibrahimu Juma na Jaji Augustine Mwarija.

Jopo hilo lilikubali hoja za warufani waliowakilishwa na mawakili Richard Rweyongeza, Majura Magafu, Barnabas Luguwa, Samson Mbamba na Gabinus Galikano kuwa Mahakama Kuu ilikosea kuwatia hatiani kwa kuwa haikuwa na ushahidi wa kutosha.