TMA: Mvua zinazonyesha sasa Dar hazitasababisha madhara

Meneja kituo kikuu cha utabiri, Samwel Mbuya

Muktasari:

  • Akizungumza na Mwananchi leo Alhamisi, Agosti 17, Meneja kituo kikuu cha utabiri, Samwel Mbuya amesema  manyunyu na mvua zinazoonekana zimesababishwa na mabadiliko ya mfumo wa hali ya hewa kama ambavyo taarifa ya hali ya hewa ya mamlaka hiyo ya Juni ilieleza.

Dar es Salaam. Kufuatia kuendelea kwa mvua za hapa na pale jijini Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA) imesema mvua hizo haziwezi kusababisha madhara kwani zinatokana na mabadiliko tu ya muda mfupi.

Akizungumza na Mwananchi leo Alhamisi, Agosti 17, Meneja kituo kikuu cha utabiri, Samwel Mbuya amesema  manyunyu na mvua zinazoonekana zimesababishwa na mabadiliko ya mfumo wa hali ya hewa kama ambavyo taarifa ya hali ya hewa ya mamlaka hiyo ya Juni ilieleza.

Amesema  Mamlaka ya Hali ya Hewa itaendelea kutoa taarifa za hali na mwenendo wa mvua hizo ili kusaidia jamii kupata taarifa muhimu kuhusiana na maendeleo ya hali ya hewa.

 Ameongeza kuwa sambamba taarifa hizo  mamlaka itatoa taarifa ya utabiri wa mvua za vuli 2017 mwishoni mwa Agosti 2017.