TRA kuwabana wenye nyumba za kupanga

Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi, Richard Kayombo

Muktasari:

Hayo yamesemwa leo na Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi, Richard Kayombo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari.

Dar es Salaam. Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) imesema kuwa itaanza kuwabana wenye nyumba za kupanga ili waweze kulipa kodi.

Hayo yamesemwa leo na Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi, Richard Kayombo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari.

Amesema watazunguka nyumba kwa nyumba kuhakikisha wapangaji wanatoa mikataba na inalipiwa kodi.