TTB yaanza kutangaza vivutio Israel

Muktasari:

Mwenyekiti wa TTB Jaji mstaafu Thomas Mihayo amesema leo kuwa mpango huo unalenga kuongeza idadi ya watalii kutoka Israel ambao wameonyesha mwamko wa kuja kuangalia vivutio vya utalii nchini.

Dar es Salaam. Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imeanza mpango wa kutangaza vivutio vya utalii vya Tanzania  nchini Israel ikiwa mwendelezo wa uhusiano wa nchi hizo mbili.

Mwenyekiti wa TTB Jaji mstaafu Thomas Mihayo amesema leo kuwa mpango huo unalenga kuongeza idadi ya watalii kutoka Israel ambao wameonyesha mwamko wa kuja kuangalia vivutio vya utalii nchini.

Amesema kwa kuanzia bodi hiyo imeandaa ziara ya siku tatu kwa watu maarufu kutoka Israel kuja kutembelea hifadhi ya Gombe.

Jopo hilo la wageni 10 litahusisha waandishi wa habari, mawakala wa kampuni ya usafirishaji watalii ya Safari Company na mwigizaji maarufu kutoka Israel anayefahamika kama Rashef Polly.