Tamasha la Ziff lazinduliwa
Muktasari:
- Uzinduzi huo umefanyika leo visiwani Zanzibar
Zanzibar. Maandamano ya uzinduzi wa Tamasha la 21 la filamu za Zanzibar (Ziff) yameanza leo jioni Jumamosi Julai 7, 2018.
Maandamano hayo yameanzia katika viwanja vya bustani ya Kisonge hadi Forodhani ambako litafanyika tamasha hilo kwa siku tisa.
Vikundi mbali mbali vya burudani vimeshiriki katika maandamano hayo huku vikitoa burudani ya aina yake kwa wageni na wenyeji.
Katika tamasha la mwaka huu, filamu 165 za wasanii mbalimbali barani Afrika zitaonyeshwa.