Uingereza yashauri uwekezaji nchini

Muktasari:

  • Kila halmashauri inatakiwa kuwa na kiwanda kimoja hususan katika maeneo yenye wanyama wengi ili kuwawezesha wafugaji kupata soko la uhakika la nyama na ngozi ndani na nje ya nchi

Watanzania wameshauriwa kuwekeza kwenye viwanda vya kisasa vya machinjio ya nyama ili viweze kuongeza thamani ya mifugo yao na kuweza kupata soko la uhakika nje ya nchi.

Hayo yalisemwa jana na Meneja masoko wa Afrika mashariki ,Gaula Willard kutoka kampuni ya Abachem Engineering ya Uingereza inayojihusisha na ujenzi wa viwanda vya machinjio ya kisasa.

Amesema kuwa, Tanzania kuna fursa kubwa Sana ya kuwekeza kwenye viwanda vya nyama kutokana na kuwa ndio nchi yenye mifugo mingi na hivyo kuna umuhimu wa kuwekeza kwenye viwanda vya machinjio ya kisasa ili kuongeza thamani ya mifugo .

Gaula alisema kuwa, wamekuwa wakitoa mafunzo kwa wadau mbalimbali kuhusu umuhimu wa kuwekeza katika machinjio ya kisasa ambapo wameweza kufunga viwanda vya machinjio ya nyama 80 duniani.

"Kwa sasa hivi tumeamua kuja Tanzania kwani kuna fursa kubwa Sana na tunataka kuleta utaalamu wetu hapa nchini kwa kuhakikisha kunakuwepo na viwanda vya kisasa Kama vya wenzetu wa nje ya nchi ambavyo Vina uwezo wa kuhudumia mifugo mingi kwa wakati mmoja kutokana na teknolojia zilizopo "amesema Gaula.