Ukumbi wa disko wa NK kugeuzwa ofisi za serikali

Sehemu ya mkoa wa Dodoma.

Muktasari:

Ukumbi huo wa ghorofa moja unaomilikiwa na CDA, uko katika Barabara ya tatu ya mtaa wa Uhindini na ulijengwa kwa matumizi ya starehe lakini sasa unalazimika kubadilishiwa matumizi.

Dodoma. Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu Dodoma (CDA) imeanza kutafuta mwekezaji wa kuboresha ukumbi maarufu wa zamani wa disko wa NK ili utumiwe na wizara au idara za Serikali.

Ukumbi huo wa ghorofa moja unaomilikiwa na CDA, uko katika Barabara ya tatu ya mtaa wa Uhindini na ulijengwa kwa matumizi ya starehe lakini sasa unalazimika kubadilishiwa matumizi.

Msemaji wa CDA, Angela Msimbira alisema jana kwamba mamlaka hiyo ipo kwenye mchakato wa kumpata mwekezaji atakayeubadilisha na kuuboresha na ili sasa jengo hilo litumika kwa  shughuli za kiserikali.