Urasmishaji wa majengo, upimaji viwanja kuongeza mapato ya Serikali

Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango akiwaonyesha wabunge begi lililobeba hotuba ya Bajeti Kuu ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 alipokuwa akiingia kwenye umbumbi wa Bunge kwa ajili ya kuiwasilisha, jijini Dodoma leo. Picha na Edwin Mjwahuzi

Muktasari:

Serikali imejipanga kuongeza mapato kwa kupanua wigo wa kodi

Dodoma. Serikali imesema itaendelea na urasmishaji wa majengo na upimaji wa viwanja ili kukuza mapato ya ndani.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango alipokuwa anasoma bajeti ya Serikali kwa mwaka 2018/19 bungeni jijini hapa.

Akieleza kuhusu sera ya mapato kwa mwaka huo wa fedha, waziri alisema serikali imejipanga kuongeza mapato kwa kupanua wigo wa kodi na kuimarisha vyanzo vilivyopo.

Katika kutekeleza hilo, alisema mkakati uliopo ni: “Kurasmisha majengo na upimaji wa viwanja mchakato unaoendelea nchi nzima.’