Viongozi wa Chadema wakamatwa, wahojiwa na Polisi Mbinga

Katibu Mkuu wa Chadema, Vincent Mashinji

Muktasari:

  • Agosti 30 mwaka jana, viongozi wa Chadema walikamatwa wakifanya mkutano katika Hoteli ya Girrafe jijini Dar es Salaam.
  • Viongozi  waliokamatwa siku hiyo ni Freeman Mbowe, Edward Lowassa, Dk Vicent Mashinji, John Mnyika na Said Issah, ambao walikuwa wakikutana na jumla ya wajumbe 170 wa chama hicho.

Songea.  Katibu Mkuu wa Chadema, Vincent Mashinji, mbunge wa Ndanda, Cecil Mwambe na wa Viti Maalumu, Zubeda  Sakuru wamekamatwa na Jeshi la Polisi wilayani Nyasa leo.

Taarifa iliyotumwa leo Jumamosi, Julai 15 kwa vyombo vya habari na Kitengo cha Mawasiliano cha Chadema, imeeleza kuwa viongozi hao wamepelekwa kituoni kuhojiwa.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, viongozi hao walivamia kikao cha ndani cha Chadema kilichokuwa kikiendelea mjini hapo ikiwa ni sehemu ya ziara ya Dk Mashinji ya kukagua shughuli za chama katika kanda hiyo.

 

Tutaendelea kuwajuza kuhusu tukio hili