Waalimu 94 kuvuliwa vyeo Dar

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Alli Hapi ameagiza walimu 68 wa shule za msingi na 22 wa shule za sekondari wavuliwe vyeo vyao kutokana na kubainika kuwa na wanafunzi hewa.

Hatua hiyo imekuja baada ya kubaini kuwapo kwa wanafunzi hewa 5000 katika shule za msingi na sekondari katika manispaa hiyo ambao wamekuwa wakipata ruzuku ya elimu bure.

Alisema baada ya uhakiki wa kubaini wanafunzi hewa ilibainika wakuu hao wa shule walifanya udanganyifu kwa lengo la kujipatia fedha za wanafunzi hao.