VIDEO: Wabunge Komu, Kubenea wawasili kikao cha Kamati Kuu Chadema
Muktasari:
Wakati kikao cha Kamati Kuu ya Chadema kikiendelea leo Jumatano Oktoba 17, 2018 wabunge wawili wa chama hicho kikuu cha upinzani Tanzania, Saed Kubenea (Ubungo) na Anthony Komu (Moshi Vijijini) wamewasili eneo kinapofanyika kikao hicho
Dar es Salaam. Wakati kikao cha Kamati Kuu ya Chadema kikiendelea leo Jumatano Oktoba 17, 2018 wabunge wawili wa chama hicho kikuu cha upinzani Tanzania, Saed Kubenea (Ubungo) na Anthony Komu (Moshi Vijijini) wamewasili eneo kinapofanyika kikao hicho.
Kikao hicho kinachofanyika katika ukumbi wa Ledger Plaza katika Hoteli ya Bahari Beach kinajadili masuala mbalimbali yanayoendelea ndani na nje ya chama hicho likiwamo la wabunge hao.
Kubenea na Komu katika siku za hivi karibuni wamezua mjadala ndani na nje ya chama hicho kwa kile kinachodaiwa ni sauti yao inayosikika wakipanga mpango hasi dhidi ya Meya wa Ubungo, Boniface Jacob.
Wabunge hao kwa nyakati tofauti wamekana kuhusika na sauti hiyo kwa kile walichoeleza ni ya kutengeneza huku Jacob ambaye ni Diwani wa Ubungo (Chadema) naye akieleza kupeleka suala hilo ndani ya chama.
Leo saa 8:01 mchana Komu na Kubenea wameshuhudiwa na MCL Digital wakiwa nje ya ukumbi huo wakisubiri maelekezo ya kuingia katika kikao hicho.
Pia, Chadema kimeonyesha magari yake aina ya Ford Ranger ambayo yatatumika katika shughuli za kukiimarisha chama hicho na kukirejesha kwa wananchi.
Msemaji wa chama hicho kikuu cha upinzani Tanzania, Tumaini Makene ameseama magari hayo yatatumika katika chaguzi na utekelezaji programu ya Chadema msingi.