Wakulima 3000 Mbeya waingia mkataba kuzalisha Pareto bora

Mbeya. Wakulima 3,000  mkoani hapa wataingia mkataba wa kilimo bora cha zao la Pareto na Kiwanda kipya cha kusindika pareto cha Tan Extracts kilichopo katika Kijiji cha Inyala , Wilaya ya Mbeya.

Lengo la mkataba huo ni kuzalisha pareto  iliyo bora na kuuza kwa bei kubwa kwenye kiwanda hicho.

Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda hicho, Zavedi Chelele aliyasema hayo jana jioni wakati wa uwekaji wa jiwe la msingi kiwandani hapo uliofanywa na Kiongozi wa Mbio za Mwenge kitaifa Amour Hamad Amour ulipokuwa katika Halmashauri ya Mbeya.

Chelele alisema hadi sasa wakulima1, 000 wa Pareto wameingia mkataba na kiwanda hicho huku lengo likiwa ni kuwafikia wakulima 3,000.