Wanyonge, maskini waathiriwa na uhaba wa dawa

Waziri wa Afya,Maendeleo ya jamii ,Jinsia, Wazee,Watoto na Walemavu,Ummy Mwalimu

Muktasari:

Hata hivyo, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ilikanusha taarifa za uhaba huo na kusisitiza kuwa zilizopo zinatosha kwa asilimia 53.

Dar es Salaam. Serikali imeshauriwa kulitazama suala la uhaba wa dawa nchini kama janga la Taifa.

Kwa muda sasa kumekuwapo madai ya uhaba wa dawa nchini, jambo ambalo wadau wa afya, wanasiasa na wanazuoni wanaeleza linawaumiza Watanzania wanyonge na maskini.

Hata hivyo, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ilikanusha taarifa za uhaba huo na kusisitiza kuwa zilizopo zinatosha kwa asilimia 53.

Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi wa Chama cha ACT -Wazalendo, Zitto Kabwe amesema tatizo la dawa ni kubwa kuliko watu wanavyodhani. Amesema ufisadi wa Sh850 bilioni wa ‘Akaunti ya Tegeta Escrow’ ni zaidi ya mara tatu ya bajeti yote ya dawa kwa mwaka.

Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa Benson Bana amesema ukosefu wa dawa nchini ni janga kama watoa takwimu hawazitoi kwa usahihi.

Mwanasheria maarufu nchini, Profesa Abdallah Safari ameitupia lawama Serikali kwa kushindwa kulinda vyanzo vya fedha na kusababisha kuwa na bajeti ndogo ya afya.