Wasaka wafanyabiashara wakubwa

Muktasari:

Lawrence amesema uamuzi huo unalenga sukari hiyo inunuliwe yote ili iweze kusambazwa kwa wananchi kwa bei nafuu. 

Tarime. Ofisa Biashara wa Halmashauri ya Mji wa Tarime mkoani Mara, Charles Lawrence amesema wanafanya jitihada kuwashawishi wafanyabiasha wawili wakubwa mkoani humo ambao watauziwa sukari ya Serikali kwa bei nafuu.

Lawrence amesema uamuzi huo unalenga sukari hiyo inunuliwe yote ili iweze kusambazwa kwa wananchi kwa bei nafuu. 

Ofisa huyo ambaye hakuwa tayari kuwataja majina wafanyabiashara hao, amesema uuzaji wa sukari hiyo unatokana na wafanyabiashara wengi kuisusia kutokana na bei ya jumla ya mfuko kuwa kubwa, hivyo kuwafanya wapate hasara. 

“Tunaamini kwa utaratibu huu wananchi watapata sukari kwa bei nafuu kabisa,” amesema.