Washtakiwa kesi ya akaunti feki ya tetemeko wapata dhamana

Muktasari:

Hata hivyo, mshtakiwa wa kwanza, Amantius Msole ambaye alikuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera, amekwama na kurudishwa rumande baada ya kukosa mdhamini wa kuaminika.

Bukoba. Mahakama ya hakimu mkazi Bukoba imewaachia kwa dhamana washtakiwa watatu wa kesi ya kufungua akaunti feki ya tetemeko mkoani Kagera.

Hata hivyo, mshtakiwa wa kwanza, Amantius Msole ambaye alikuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera, amekwama na kurudishwa rumande baada ya kukosa mdhamini wa kuaminika.

Wametakiwa wasalimishe hati za kusafiria, kuwa wadhamini wawili kila mmoja anasaini bondi ya Sh5 milioni na hawaruhusiwi kutoka nje ya mkoa wa Kagera. Kesi itatajwa Oktoba 13.