Watatu wazama Ziwa Victoria

Muktasari:

  • Watu hao ambao majina yao bado hayajajulikana, walikuwa wakivua samaki katika eneo la Kyagalanyi lililopo kusini mwa Uganda upande wa Ziwa Victoria.

Kuna ripoti kuwa wavuvi watatu wamepoteza maisha baada ya boti waliyokuwa wakitumia kuzama maji katika Ziwa Victoria.

Watu hao ambao majina yao bado hayajajulikana, walikuwa wakivua samaki katika eneo la Kyagalanyi lililopo kusini mwa Uganda upande wa Ziwa Victoria.

Mmoja wa watu aliyekuwa karibu na tukio, Ivan Ssendijjo alilimbia gazeti la Monitor la nchini humo kuwa wavuvi hao walikuwa wamekwenda kufuata nyavu walizozitega ziwani na ndipo walipopigwa na upepo mkali na kusababisha boti yao kupotea.

“Tulijaribu kwa kadri ya uwezo wetu ili kuwaokoa, lakini hatukuweza kufanikiwa kutambua sehemu waliyopotelea,” amesema.

Ofisa wa polisi katika eneo hilo, Ivan Tenywa amewaambia waandishi wa habari kuwa wamefanikiwa kupata miili ya wavuvi wawili, huku mwingine akiwa bado hajaonekana.

Tukio hilo limetokea siku chache baada ya watu wengine sita kuokolewa na mashua ya polisi wakati boti yao ilipozama katika ziwa hilo