Waziri Lukuvi azua taharuki mazishi ya Ndesamburo

Muktasari:

 Hali hiyo ilisababisha hofu kwa wananchi wengi waliokuwa nje ya   kanisa hilo na baadhi wakishindwa kuingia kanisani katika ibada iliyokuwa inaendelea ndani.

Katika hali isiyo ya kawaida Waziri Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi , Wiliam Lukuvi jana alizua taharuki baada ya kuwasili katika ibada ya mazishi ya aliyekuwa mbunge wa jimbo la Moshi Mjini Philemon Ndesamburo akiwa ameongozana na magari mawili ya polisi waliobeba silaha.

Ibada hiyo ilifanyika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) usharika wa Kiboriloni mjini Moshi jana.

Hali hiyo ilisababisha hofu kwa wananchi wengi waliokuwa nje ya kanisa hilo na baadhi wakishindwa kuingia kanisani katika ibada iliyokuwa inaendelea ndani.

Hata hivyo ni kawaida kwa waziri kuongozwa na vyombo vya usalama wakati wa msongamano wa watu.