Waziri Nchemba awasili eneo yalipotokea mauaji ya polisi wanane

Muktasari:

Waziri Nchemba ameambatana na naibu wa wizara hiyo, Mhandisi Hamad Masauni.


Dar es Salaam. Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba amewasili eneo yalipotokea mauaji ya askari wanane katika kijiji cha Jaribu, Wilayani Kibiti.

Waziri Nchemba ameambatana na naibu wa wizara hiyo, Mhandisi Hamad Masauni.

Nchemba atatembelea kambi za askari polisi wa kanda ya Pwani na katika kata ya Bungu wilayani Kibiti.