Waziri aivunja Bodi ya soko la Kariakoo

Muktasari:

Uongozi huo ulipewa jukumu la kumshauri Waziri wa Tamisemi lakini imeshindwa kufanya hivyo

Waziri wa Nchi Ofisi  ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa George Simbachawene ameivunja bodi ya Shirika la Masoko Kariakoo baada ya kushindwa  kutekeleza majukumu yake ya msingi.

Taarifa kwa vyombo vya habari iliyosainiwa na Msemaji wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Rebecca Kwandu ilisema kwamba  uamuzi huo ni baada ya uongozi kushindwa kutekeleza majukumu yao ya msingi waliyopewa ya kumshauri Waziri wa Nchi Tamisemi juu ya uendeshaji wa Soko hilo.