Sababu tano kwa nini uchague mtandao wa Telegram

Muktasari:

  • Lakini zifuatazo ni faida tano za kukufanya uuchague mtandao wa Telegram ambazo huwezi kuzipata kwingine.

Karibu kila mwenye ‘smartphone’ anatumia ‘application’ ya WhatsApp. Hii inatajwa kuwa programu ya mawasiliano kwa njia sauti, video na ujumbe wa maandishi yenye watumiaji wengi zaidi duniani.

Lakini zifuatazo ni faida tano za kukufanya uuchague mtandao wa Telegram ambazo huwezi kuzipata kwingine.

Uhifadhi wa mtandaoni

Telegram huhifadhi vitu mtandaoni na si kwenye simu

Tuma faili la ukubwa hata wa GB 1.5

Kwa watu wanaotumia WhatsApp wanafahamu kwamba huwezi kutuma faili lenye ukubwa wa kuzidi MB 16 kupitia mtandao huo.

 

Mawasiliano ya siri

Hii ni aina ya kutumiana meseji ambayo watumiaji wanakuwa wanaweka muda wa kufutika kwa mesjei zao, na muda unapofikia, meseji hujifuta zenyewe, na zinapofutika, hakuna namna ya kuziona tena.

 

Kundi la wanachama hadi 5,000

Kwa njia ya kawaida, kundi la WhatsApps linaweza kubeba wanakikundi 256 tu. Wakati kwenye Telegram, kundi lina uwezo wa kuwa na idadi ya wanachama hadi 5,000 na zaidi katika Super Groups.

 

Kujisajili bila namba

Kama ambavyo ni lazima kujisajili kwa kutumia nambari ya simu kwenye WhatsApp, ndivyo unavyoweza kujisali kwenye Telegarm pia.