|
Uchaguzi 2010 Ahadi za wagombea urais |
Send to a friend |
|
Friday, 15 October 2010 12:30 |
|
 | Ahadi za Kikwete: 1. Kujenga reli mpya kutoka Dar es Salaam mpaka mikoa ya Kanda ya ziwa-Nzega, Tabora - Mkoa wa Tanga kuwa Jiji la Viwanda- Tanga mjini
- Tabora kutumia maji ya Ziwa Victoria-Igunga
- Kulipa madeni ya chama cha Ushirika mkoa wa Shinyanga (SHIRECU)- Shinyanga
- Kumaliza migogoro ya Ardhi nchini- Dodoma
- Wakulima kuacha kutumia jembe la mkono-Dodoma mjini
- Kuwapatia trekta wakulima -Kata ya Mrijo, Dodoma
- Wananchi kutoondolewa kwenye Ranchi ya Misenyi-Kagera
- Kujenga Uwanja wa Ndege Misenyi-Kagera
- Kupanua Uwanja wa Ndege Bukoba-Bukoba Mjini
- Kujenga uwanja wa ndege mkubwa Kigoma - Kigoma Mjini
- Mtukula kupatiwa umeme kutoka Uganda- Kagera
- Mikoa ya Kagera, Kigoma, Lindi, Rukwa na Ruvuma kuunganishwa katika gridi ya taifa ya umeme- Kagera
- Kuimarisha Takukuru kwa miaka mitatu-Kagera
- Hukumu kwa waliopatikana na hati ya kuua albino- Mbeya
- Kununua meli kubwa kuliko MV Bukoba-Kagera
- Kuanzisha benki ndogondogo kwa ajili ya wajasiriamali
- Serikali kuvisaidia vyama vya ushirika-Mwanza
- Kuimarisha usalama Ziwa Victoria na Ziwa Tanganyika kwa kupeleka kikosi maalum chenye vifaa kupambana na wahalifu-Mwanza
- Wilaya ya Geita kuwa hadhi ya mkoa Januari mwakani- Geita
- Kulinda muungano kwa nguvu zote-Pemba
- Kuwajengea nyumba waathirika wa mafuriko Kilosa-Morogoro
- Kununua meli mpya kubwa Ziwa Nyasa-Mbeya mjini
- Kujenga bandari Kasanga –Rukwa
- Kumaliza tatizo la walimu miaka mitano ijayo - Songea
- Kufufua mgodi wa makaa ya mawe Kiwira -Mbeya
- Kuzuia hatari ya kisiwa cha Pangani kuzama- Tanga
- Kununua bajaji 400 kwa ajili ya kubeba wajawazito hasa vijijini- Iringa
- Kujenga barabara yenye kiwango cha lami kutoka Same mpaka Kisiwani –Kihurio na kuiunganisha na barabara kuu ya Moshi -Dar es salaam- Same mkoani Kilimanjaro
- Kumaliza tatizo la maji katika wilaya ya Same-Same Mjini
- Kuboresha barabara za Igunga -Tabora
- Kusambaza walimu 16,000 katika shule za sekondari zenye upungufu makubwa wa walimu- Kisesa Magu
- Kununua vyandarua viwili kwa kila kaya- Mbeya Mjini
- Kuzipandisha hadhi hospitali maalumu saba nchini kuwa za rufaa ili kuipunguzia mzigo Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MHN)-Hydom Manyara
- Kulinda amani nchini kwa kuzuia chokochoko za kidini, kikabila na kisiasa- Musoma
- Kulinda haki za walemavu- Makete
- Kujenga baabara ya Njombe- Makete kwa kiwango cha lami,urefu wa kilomita 109- Iringa mjini
- Kujenga barabara Musoma–Mto wa Mbu Arusha-Arusha
- Kuanzisha jimbo la Ulyankulu- Shinyanga Mjini
- Kujenga barabara ya lami Manyoni-Kigoma– Kaliua,Tabora
- Kukarabati barabara ya Arusha Moshi-Arusha Mjini
- Kuboresha barabara ya Handeni, Kondoa,mpaka Singida-Dodoma
- Kuwafidia wanakijiji ng’ombe waliopotea wakati wa ukame mwaka 2009- Longido 45.Vijiji vyote vilivyoko kilomita 15 kutoka kwenye bomba kuu la mradi mkuu wa maji wa Ziwa Victoria-Shinyanga-Kahama kuunganishiwa maji - Shinyanga
- Tatizo la umeme kufikia kikomo Novemba mwaka huu mkoani Arusha –Arusha mjini
- Kukopesha wavuvi zana za kilimo-Busekera, Wilaya ya Musoma, .
- Kuwapatia maji wakazi wa Wilaya ya Longido- Longido
- Kujenga barabara ya lami kupitia pembezoni mwa Hifadhi ya Taifa ya Seregenti – Ngorongoro
- Utekelezaji wa mpango wa maendeleo ya kilimo kuwasaidia wafugaji kuweza kupata na kutunza mifugo yao vizuri- Mbulu mkoani Manyara
- Kusambaza maji nchi nzima-Babati vijijini
- Kusambaza umeme, utoaji wa huduma za afya, na uboreshaji wa kilimo cha umwagiliaji na utoaji ruzuku kwa wakulima. mwaka 2010-2015-Babati vijijini Kuongeza mara tatu idadi ya wananchi wanaonufaika na ruzuku ya pembejeo za kilimo kwa mfumo wa vocha.-Iringa
- Kuhakikisha Isimani inapata maji ya uhakika- Iringa
- Kuiwekea lami barabara inayokwenda katika Hifadhi ya Taifa ya Ruaha, ambayo ndiyo hifadhi kubwa kuliko zote Tanzania-Iringa
- Kulinda usalama wa wananchi kwa ujumla ili kudumisha amani na sifa ya nchi-Ifunda
- kutokomeza malaria 2015-Bunda,mkoa wa Mara
- kuwapa wanawake nafasi zaidi-Kilolo ,Iringa
- ahadi kuisadia Zanzibar kuendeleza miradi mbalimbali ya kijamii-Kibandamaiti Mjini Zanzibar
- Kuipandisha hadhi hospitali ya Mnazi Mmoja Zanzibar kuwa ya rufaa-Kabandamaiti mjini Zanzibar
- Kuisaidia Zanzibar kila panapohitajika msaada-Kibandamaiti
- Serikali kujenga upya bandari ya Mbambabay-Ruvuma
- Ununuzi wa Meli mpya yenye uwezo wa kubeba tani 400-Mbambabay Ruvuma
- kufufua chama kikuu cha ushirika cha wakulima wa Mbinga(MBICU) –Ruvuma
- Ahadi Rais wa Marekani Barack Obama kuimwagia misaada Tanzania –Ruvuma
- Ahadi hakutakuwa na umwagaji wa damu baada ya uchaguzi-Dar es Salaam
- Mtwara kuwa mji wa Viwanda –Mtwara
- Ahadi ujenzi wa kwanda cha dawa ya kuua viluilui vya mbu-Kibaha
- Hospitali ya Tumbi kuwa ya mkoa-Kibaha
- Halmashauri ya manispaa ya Kibaha kutenga eneo maalumu la viwanda -Kibaha
|  | Ahadi za Dk Slaa: 1.Kujenga nchi isiyo na ufisadi 2.Kufufua Tanganyika ili irejee mezani kujadili muungano na Zanzibar 3.Kufufua uchumi wa nchi kwa kutumia rasilimali zilizopo 4.Kukata asilimia 20 ya mshahara wa rais 5.Kupunguza mishahara ya wabunge kwa asilimia 15 6. Kuweka Mwenge wa Uhuru Jumba la Makumbusho 7. Kutoa huduma bora za afya bure 8. kufuta kodi ya vifaa vya ujenzi 9. Kuwalipa wazee wa EAC fedha zao ndani ya siku 100 10. Kubana matuzi Ikula (Yuko tayari kula mihogo ) | | 
| Ahadi za Profesa Lipumba na Maalimu Seif: 1.Elimu ya bure kuanzia msingi hadi chuo kikuu 2.Kubana matumizi kwa kupunguza ukubwa wa baraza la mawaziri 3.Kuunda serikali shirikishi 4.Kusimamia rasilimali 5.Kuimarisha miundombinu 6. Kusimamia na kuboresha afya 7. Kuboresha kilimo, viwanda na uwekezaji 8. Kurudisha chakula cha bure mahospitalini
|
Maalimu Seif Sharif Hamad 1. Zanzibar kuwa kama Hong Kong – Unguja 2.Kuendeleza mashamba ya Karume- Kibanda maiti 3. Kubadilisha katiba na kuunda katiba mpya ya muungano na Zanzibar- Pemba 4.Kubadilisha mfumo wa uteuzi makamishna wa tume ya uchaguzi Zanzibar (ZEC)- Unguja 5. Kuwaunganisha wazanzibari ili kujenga umoja, udugu na ushirikiano-Pemba 6. Kuwasilisha hoja ya kubadili katiba ya Zanzibar na ya Muungano-Viwanja vya Kibanda Maiti 7. Kuondoa bajeti ya ZEC isiwe chini ya waziri kiongozi na badala yake kuwa inajitegemea yenyewe- Pemba 8. Kuondoa ulazima wa mwenyekiti wa tume kuwa jaji na badala yake awe mtu anayejua sheria-Unguja 9. Serikali kuundwa na vyama vyote vilivyopata ridhaa ya kuchaguliwa na wananchi- Unguja 10.Kujenga jamii yenye maelewano na umoja -Pemba 11.Kutokochagua kiongozi kwa urafiki bali kwa uwajibikaji na uadilifu -Unguja na pemba 12.Kudhibiti vyombo vya dola vinavyofanya kazi kwa matakwa ya watu binafsi -Kibanda maiti 13.Kukomesha rushwa-Mkanyageni Mkoa wa Kusini Pemba 14.Kuhakikisha ununuzi wa zabuni unakuwa wazi na wananchi kuruhusiwa kuhoji kuhusu zabuni-Jimbo la ole Pemba 15.Kuongeza kima cha chini cha mshahara hadi Sh150,000-Mkanyageni Pemba 16.Kubadili vikosi vyote vya usalama na kulipwa mishahara kima cha chini kulipwa Sh180,000-Chakechake Pemba 17.Kubadilisha kikosi cha KMKM kuwa kikosi cha mwambao-Wawi 18.Wazee kupanda daladala bure na wale wasiokuwa na watoto kulelewa bure-Majimbo ya Chakechake 19.Kufuta michango yote ya shule za msingi na sekondari, kila mwanafunzi kuwa na kompyuta na badala ya kuishia darasa la saba sasa kuishia kidato cha sita-Hoteli ya Bwawani 20.Kutoa kitambulisho cha kila Uzanzibari na kufuta cha Mzanzibari mkaazi- Uwanja wa Hospitali ya Mnazi Mmoja 21.Kila mzanzibar kupata pasi ya kusafiria- Hoteli ya bwawani Zanzibar 22.Kuanzisha shirika la ndege Zanzibar -Viwanja vya Kibanda maiti 23.Kupandisha uchumi wa Zanzibar kutoka 6.8 hadi 15 kila mwaka kwa Zanzibar -Unguja 24.Kutoa uhuru zaidi kwa vyombo vya habari pamoja na kusaidia uanzishwaji wa Baraza la Habari Zanzibar-Unguja na Pemba 25. Kuweka hadharani nambari yake ya simu - Viwanja vya Kibanda miti 26. Kubadili sheria ya uwekezwaji-Hospitali ya Mnazi Mmoja Zanzibar 27.Kila mwanafunzi kuwa na komputa yake-Viwanja vya Kibanda maiti 28.Akiwa rais hata waziri au mkewe atafungwa akiwa ametenda kosa-Viwanja vya Tibirizi Kisiwani Pemba 29.Kujenga bandari ya Mkokoto na Pemba ili kuweka usafiri wa haraka wa boti ziendazo kasi-Tibirizi Kisiwani Pemba 30. Ahadi kudhibiti kuvuja kwa mitihani- Unguja Dk Mohammed Shein 1) Kuboresha maisha ya wavuvi-Chakechake Pemba 2) Kusomesha wafanyakazi-Mnazi mmoja 3) Kipaumbele katika elimu -Unguja na Pemba 4) Kipaumbele katika afya-Makombeni Mkoa wa Kusini Pemba. 5) Kuulinda Muungano- Wawi kisiwani Pemba 6)Kuleta mabadiliko Zanzibar-Pemba na Unguja 7)Kuboresha Bandari ya Zanzibar kwa kuijenga upya-Kibandamaiti 8)Kuboresha Maendeleo Zanzibar- Jimbo la Wete, Pemba 9.Ujenzi wa maktaba kubwa na nzuri Kisiwani Pemba- Mtambwe 10.Kutokomeza ugonjwa wa kipindupindu Zanzibar- Kijiji cha Kambini Mchangamdogo 11.Kuimarisha miundombinu Kisiwa cha Pemba- Kijiji cha Makombeni Mkoa wa Kusini Pemba 12.Kuhamasisha wawekezaji kuwekeza Pemba katika miradi mbalimbali-Makombeni Mkoa wa Kusini Pemba. 13.Ahadi eneo la Micheweni kuwa maeneo huru ya uchumi- Micheweni Kaskakzini Pemba 14. Kumaliza matatizo ya maji mkoani -Mkoani 15..Kujenga Bandari ya kisasa katika eneo la Mpiga Duri Unguja- Mkoani 16.Kuiamrisha makazi bora kwa Wazanzibar- Mkoani
|
|
Last Updated on Thursday, 21 October 2010 16:44 |
Comments
Mungu atubariki, tunaye mtetezi wetu wa haki.
J. Nyanda
MunguIbariki Tanzania kutana na viongoziwote wafungue macho waweze kusikiliza maoni ya wananchi wanaowaongoza!
Ombi langu lingine kwa mteule na wote walioko madarakani wanaoweza kutoa tamko au maamuzi ya nani awajibike wapi! Naomba na nasihi saana yafuatayo:
Majimbo yote yenye utata wa matokeo ya ubunge naomba yafanyiwe kazi hofu yangu kubwa ni kwa yule mbunge asiye na ridhaa ya wananchi atasaidiaje au atawawakilisha vipi wananchi katika jimbo lake??? mfano Segerea, Kahama , Buchosa, Tarime, Kibaha na huko Lindi!
Tusaidiane ndugu zangu na kama nisemayo hamyaamini basi Mungu hafichwi jambo kuna siku mtakuja sema kuna mtu mmoja alisema jambo hili na likapuuzwa!
Malamiko ya mgombea urais kupitia CHADEMA nayo yasitupwe yachunguzwe zaidi pamoja na Rais mteule katangazwa sio mbaya kuweka bayana ili kufuta madukuduku ya wananchi.
Ushabiki wa waandishi nao uangaliwe maana wanawezakuandik a mambo kwa kuchanganya habari na kuchanganya wananchi, mwandishi mzuri ni yule anayeandika ukweli na hata akiulizwa aweze kutoa ushahidi.
Kwa [NENO BAYA]lizia nawatakia Baraka njema matumaini yangu makubwa Mungu wetu atasimamia yote yaliyombele yetu!
Mungu Ibariki Tanzania, Bariki Bunge jipya na ahadi za kampeni zitimizwe! mteule aliahidi mambo 68 yaliyikuwa yakitangazwa na vyombo vya habari na niliyoyaona katika ukurasa huu mtukufu.
Amani ya Bwana ikae nasi sote!
J Nyanda
TUME YA UCHAGUZI ISIKIE KILIO CHA WAANDISHI WA HABARI ( MKUTANO WA 4/11/2010) WALIKUWA WAKIULIZA NA KUTOA USHAURI KUHUSU TUME KUTEULIWA SERIKALI NA IMETEULIWA NA CHAMA AMBACHO NACHO KIMO KWENYE MCHAKATO WA KUCHAGULIWA! NI LAZIMA KIMPENDELEE BOSI WAKE BASI NA IWE "TUME HURU" IKIWEZEKANA BUNGE LIPITISHE KAMATI AU KURUGENZI YA TUME YA UCHAGUZI.
SWALA LA DR W. SLAA LISIPUUZWE TANZANIA TUMEJALIWA AMANI SIONI SABABU YA KUKIMBILIA KUAPISHA MSHINDI WAKATI KUNA UPANDE UMELETA LALAMIKO!! NI HERI TUCHELEWESHE KUMWAPISHA MTEULE TUMALIZE TATIZO, NCHI NI YETU WANOTAWALIWA NI WANANCHI, PAKIWA HAPANA MWAFAKA ITAKUWAJE?? MTEULE UTAKUWA NA RAHA GANI YA KUTAWALA WATU WENYE DUKUDUKU?? HATA KAMA UKWELI UKIJULIKANA NA TUKACHUKUWA MWEZI AU WIKI ZAIDI KUFIKIA MWAFAKA KUNA TATIZO GANI?? AU WATASOMBWA WATU KUTOKA MIKOANI KUJA KUSHIRIKI MTEULE KUAPISHWA?? TUWEKE MAMBO SAWA ILI TUFURAHI PAMOJA! UPINZANI UPO KWA AJILI YA KUWEKA CHANGAMOTO ILI KUENDELEZA NCHI YETU KIMAENDELEO NA KUDUMISHA AMANI NA SIO KUNYANYASA NA KUWANYANYAPAA!! DAIMA TUKUMBUKE WOSIA WA BABA WA TAIFA! ASANTE MUNGU KIPINDI CHOTE CHA KAMPENI HOTUBA ZAKE ZILIKUWA ZIKIWEKWA NA WATU WAMESIKIA NA YOTE YANAYOTENDEKA NCHINI SIO MAGENI NA WATANZANIA SIKU HIZI WAMEAMKA WANAJUA MBIVU NA MBICHI PUMBA NA KILICHOBORA!! NAIPENDA SANA NCHI YANGU NI MZALENDO HALISI MWENYE UCHUNGU SAANA NIKIONA MAMBO HAYAENDI SAWA!! NATAMANI MAONI HAYA YANAYOTOLEWA KATIKA UKURASA HUU WATU WASOME NA WAHUSIKA WAJIREKEBISHE KWELI TUWE NCHI YA AMANI NA UPENDO NA USAWA!! UNAJUA UWONGO UKIWA KARIBU NA UKWELI WATU HUMEZEA LAKINI UONGO UKIZIDI HATA [NENO BAYA] ANAGUNDUA!!
MUNGU AWAFUNIKE WOTE WENYE MAPENZI MEMA NA NCHI HII, AWAFUNGUE MACHO WALE WALIOZIBWA MACHO NA KUWA HAWAONI TENA KUWA WAFANYACHO HATA MUNGU ANAKASIRIKA!!
HEBU TUSIMKASIRISHE MUNGU AKALETA GHARIKA KAMA LA SODOMA NA GOMORA!!
MMBARIKIWE,
J NYANDA
kama hawa chama cha majangili hawaja chakachua kura zetukuogopa aibu?
Chakusikitisha, wakati wa kusubiri matokeo wengi wamekuwa makini kama tulivyokuwa tunasema "Hadi kieleweke" yaani kukaa na kusubiri matokeo baada ya kura. Mambo yamekuwa tofauti, sehemu zilizokuwa na upinzani mkali matokeo yamecheleweshwa hata kuelekea kuvuruga amani tuliyozowea TZ! Haki ya mtu daima haiibiwi mimi naomba tukubaliane na ukweli watu wanamwamko na wanataka mabadiriko na wanachagua wampendae. iweje matokeo yanakuwa tofauti!!! habari zinazotangazwa kuhusu matokeo kweli Mungu mwenyewe ajidhihirishe ukweli ujulikane!maana kuna matokeo yanayotolewa yanazidi hata idadi ya wapiga kura wa sehemu husika!! au jimbo limechukuliwa za chama cha upinzani lakini kura za urais na wabunge zinakuwa tofauti ina maana wapiga kura wampigie diwani tu na rais , mbunge awe tofauti? Kuna kituo Dar kililalamika kuwa iweje tulikubali kuwa na vyama vingi,iweje tukipenda kuwapa wapinzani inakuwa na tatizo?? Tanzania ni yetu,na tunachochaguwa ni wakutuwakilisha katika vyombo vya maamuzi na kutuwakilishia wananchi na wananchi tuwatume shida zetu mjengoni.
Mara zote mazungumzo ni mazuri kwa pande mbili zilizokaa na kuongelea maswala yao kwa umakini ili kufikia mwafaka! sasa itakuwaje kupa[NENO BAYA] kiongozi katika jimbo asiyekubalika? wananchi wataongea nae vipi ili awe mwakilishi wao?
asante Mungu Ibariki Tanzania
J. Nyanda
wapi?.
Mie yangu macho.