MwanzoContactsEmail
Home Makala Starehe Rafiki yako anapokusaliti unamchukulia hatua gani?
BOOKMARK THIS PAGE
Rafiki yako anapokusaliti unamchukulia hatua gani?  Send to a friend
Saturday, 28 January 2012 09:36

Herieth Makwetta
KATIKA mambo ambayo huwa magumu katika kuyafanyia maamuzi, ni kwa upande wa mpenzio na rafikiyo. Hawa wote ni  watu wa aina moja kwa kuwa si ndugu zako bali ni watu wako wa karibu.

Lakini ni wazi kuwa upendo huzidi kwa mpenzi zaidi na si rafiki. Katika maisha ya kila siku huenda siku moja rafiki yako akatongoza au kutongozwa na mpenzi wako, naye bila hiyana akakubali je utajisikiaje pindi utakapogundua umesalitiwa baina ya hawa watu wako wa karibu? Swali la wiki lilihoji

"Ukigundua kuwa mpenzi wako ana mahusiano ya kimapenzi na rafiki yako wa karibu utachukua hatua gani?" Wengi walichangia.

Fia Bright
Wape nafasi kwa kuwaambia, kwanza watasikia aibu, pili lazima aibu iwafanye wajutie!

 Pax Joseph
Utakaa chini ujue tatizo liko wapi.

Keytone Allen
Waache waendelee, maisha ni mafupi sana yafurahie..

Grace De Gregory
Siwezi kusema naogopa ushahidi

Habiba Charles
Dah inauma sana bora nisigundue! iwe siri yake na huyo best friend wake.

Sebastian Shirima
Mimi nampiga chini tu ndilo lililobaki.

Pendo A Sanga
Mimi nitamwambia jamaa kuwa hapaswi kunifanyia hivyo mimi mwanaume mwenzake kwani "ukisosombola vya wenzako na vyako watakusosombolea"

Habiba Charles
Mwachie akaangaike weeee lakini jioni lazima akirudishe nyumbani.

Lissa Massala
Penzi likishaisha hakuna jinsi, waache wafurahie penzi lao, lakini kuwaambia ukweli ni lazima.

Oltesh Shange
Na ukiwacha huoni kama utaumia sana? Ila usilazimishe mapenzi pasipo na penzi! Moyo wangu ni mwepesi sana kukubali matokeo! Huwa naamini kama kuna mwanzo, basi na mwisho pia upo!

Gati Saimon
Hata umpe nini, penzi likiisha huna jinsi!! Watu wanapewa gari, nyumba na nyama ya ulimi mpaka anatapika, lakini bado anatoa penzi kwa muuza mkaa!

Mujuni Gaulah Kajala
Mapenzi siyo ya kuyachukulia kirahisi kihivyo, ndiyo maana watu tunamwagana kila siku.

Emanuel S Mrindoko ?
Mbona rahisi sana katika hilo unasamehe ushaibiwa na wewe unaenda kuiba .

Janeth Mwenda
Wahenga walisema 'Penzi la mama haliishi' lakini sio hayo mapenzi yenu ya kisasa, yanaisha na kusahaulika kabisa!

Gabriel Mathew Nsangaluf Jr.
Ukimegewa wako nawe tafuta mnyonge ummegee.

Upupu Limitedi
Inabidi hapo ujimwilike wewe kwanza unaweza kuta wewe ndio chanzo cha tatizo

Martin Jofrey G
Lazima kuna mapungufu mahali! inabidi kujichunguza upya.

Halima Lameck
Ni kuachana nae kwani hatakua na mapenzi ya kweli
          
James Victory
Nitashukuru sababu atakuwa amenifundisha kuwa nina mapungufu sehemu fulani pia nitawaacha waendelee.


Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner