MwanzoContactsEmail
Home Makala Starehe Ukubwa pesa, ..ndevu uzee tu!
BOOKMARK THIS PAGE
Ukubwa pesa, ..ndevu uzee tu!  Send to a friend
Saturday, 28 January 2012 09:39

Hivi ushawahi kuibuka Moshi mwisho wa Mwaka? Kuna washua na midevu yao unaambiwa huwa wanawaamkia watoto wao wakirudi kutoka tauni kuzisaka, nje nje unaambiwa bila noma wala nini unakuta zee la kichagga linamwambia mwanawe,

"Shikamoo mwanangu!"
Heshima kudadadeki kwa jinsi dogo alivyochakarika na kuleta mafanikio nyumbani lakini nikirudi kwetu pwani, heshima iko tofauti, mtu mwenye ndevu, hasa zile zinazoelekea katika kubadilika rangi ndio tunamheshimu, na ndio maana mpaka ile ngoma ya tanga kunani ikaimbwa na wagosi...

Sipondi kwetu lakini hizi ishu za kuchakarika kwa nini ziko kwenye baadhi ya makabila halafu kwetu kunadorora, maana ukisikia duka ujue ni kwa Mangi, makabila mengine wachaaaahe sana au kwa mpemba, ina maana sisi wazigua tumeshinfdwa kuwa na maduka?

Hatuna hela au hatujui biashara?
Natamani kupata taimu niibuke, kitaa cha homu kwetu, kule vileji kabisa nikakutane na washua wale, ...wenyewe kabisa niwaulize, hivi ilikuwaje mpaka sisi tunakuwa kama maboya tu kule tauni?
Hili kabila lilimkosea nini Mungu?

...imenitachi sana hii na imekuja kutokana na ishu moja hivi niliisikia kitaa, ilikuwa kama sio ya ukweli hivi lakini pia inatoa fundisho ikiwekwa kwenye masomo kama haya ya kitaa.
Uliza ilikuwaje?
wanaotumwa madukani mara nyingi wanakuwaga masista zetu, hii haina ubishi na sasa, mshua mmoja kule Tanga unaambiwa alikuwa mara kwa mara akikitumia kibinti chake aidha kwenda kununua bishaa lakini wakati mwingine pian kilikuwa kikiibuka kwa mtu mzima Mangi kwenda kukopa.
Unaona bwana?

Urafiki ukajengeka nini, ..mangi akaziingiza kwa mtoto, na mtoto kwa kuwa alishaona picha kwamba bila huyu mchizi homu kitakuwa hakieleweki, ..akaingia laini, kale kamchezo kakaanza!

sasa si unajua zile mambo zetu zikianza? Binti sasa ikawa akitumwa kwa Mangi anachukua hata lisaa kumaliza mambo yake na mara nyingi akawa akiulizwa, anachojibu ni kwamba Mangi alikataa na alikuwa katika hatua za kumsomesha ili aelewe.

Dingi akiambiwa hivyo tu unaambiwa ana'kulu dauni'.
lenye mwanzo kwani linakosa mwisho mwanangu?
..siku mbili tatu binti akawa kama keshashiba mahaba ya mangi hivi na katoto kama kanaanza kusumbua tumboni hivi, dingi unaambiwa akashtukia lakini sasa kumvaa Mangi anaanzaje wakati Mangi ndio mpango mzima kwenye fanmilia?

Inambidi achune tu, lakini moyoni anaumia binti kaharibiwa maisha, shule ndio ikawa basi tena, na mangi ndio humuelezi kitu.

We umepata picha gani hapa? Kama mshua angekuwa mtu wa kuchakarika unafikiri angekosa nguvu ya kumvaa Mzee Mangi?

Lazima angeenda kumzingua lakini kwa sababu alikuwa mtu wa kuskilizia acha ya mkute na binti ndio alikuwa jembe homu inabidi akalime kahawa moshi na mshua aendelee tu kukopa kwa Mangi na ipo siku ujue mangi atachoka, atakodi fremu mbali na pale atasepa!

Acheni kufuga ndevu wanangu mwaka ndio huu, tutafuteni mkwanja sawa?
Wanlav...


Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner