MwanzoContactsEmail
Home Makala Jungukuu Kulikoni Serikali inapata hasara Sh300bilioni kwa uchakachauji, wahusika wanaachwa?
BOOKMARK THIS PAGE
Kulikoni Serikali inapata hasara Sh300bilioni kwa uchakachauji, wahusika wanaachwa?  Send to a friend
Thursday, 02 September 2010 14:17


Lauden Mwambona
MKUU wa Mkoa wa Shinyanga, Brigedia Jenerali Mstaafu, Dk Yohana Balele hivi karibuni alinukuliwa akisema  serikali imepoteza Sh300 bilioni kutokana na uchakachuaji wa mafuta.

Hasara ya fedha hizo ni kwa mwaka wa fedha 2009/2010 pekee. Uchakachuaji ni uchanganyaji wa mafuta ya dieseli au petroli pamoja na mafuta ya taa.

Lengo la watu wanaochanganya mafuta hayo ni kutaka kupata faida kubwa zaidi licha ya kwamba mchanganyiko huo unaharibu mitambo ya aina mbalimbali ikiwemo ya magari, pikipiki, mashine za kusaga, mashine za kuvuta maji na mingine mingi.

Wafanyabiashara hao wanachanganya mafuta ya petroli na mafuta ya taa kwa sababu bei ya mafuta ya taa ni Sh1,000 kwa lita wakati mafuta ya Dieseli au Petroli ni zaidi ya Sh1,600, hivyo akichanganya mafuta hayo anaona atafaidika.

Uchakachuaji huo unadaiwa kushamiri kwenye vituo vingi vya mafuta ambavyo vingi vimejengewa ukuta ili kuficha mambo yanayofanyika ndani. Vituo vipo kuanzia Dar es Salaam hadi Mbeya,  hadi Arusha, hadi Mwanza na hadi Mtwara ama Songea.

Athari za uchakachuaji mafuta zimefika hadi Ikulu ambako magari ya Rais yalionja adha kule Kilimanjaro katika mji wa Moshi ambako yalizimika muda mfupi baada ya kuwekezwa mafuta ambayo yalidaiwa kuchakachuliwa.

Pamoja na suala hilo kupiga hodi Ikulu, hatua zilizochukuliwa ni kukifungia na  kulipa faini.
Dk Balele ambaye bila shaka  anayo mengi ya kusema juu ya suala hilo alilazimika kueleza tena suala hilo  kwenye uzinduzi wa Kamati ya Mkoa ya Baraza la Ushauri la Watumiaji wa huduma zinazothibitiwa na Ewura.

Lakini ukweli ni ni kwamba mkuu huyo wa mkoa alitoa takwimu hizo akinukuu hotuba ya Waziri wa Nishati na Madini Walliam Ngeleja aliyoitoa kwenye kikao cha Bunge la Bajeti Julai mwaka huu.

Mwanajeshi huyo aliongeza kwamba uchakachuaji ni mchezo mchafu, ni kuhujumu uchumi wa Taifa, lakini akaliachia kazi Baraza husika kukabiliana na vitendo hivyo.

Hoja ya msingi ni je  Baraza kama hilo ndilo linatakiwa kupambana na wahujumu uchumi?  Je  kwa kitendo cha serikali kukwepa majukumu yake , biashara ya uchakachuaji  ni ya serikali ama wafanyabiashara?  Inakuwaje  Rais aonje joto la jiwe kwa uchakachuaji , lakini wasikamatwe wafanyabiashara husika wote kwa kuhojiwa?. Ni kwa vipi Serikali ipate takwimu za hasara ya Sh300 bilioni, lakini wanaosababisha hasara wasikamatwe ?
Mkuu wa mkoa anasema wazi kwamba uchakachuaji ni uhujumu uchumi, je ni wafanyabiashara wangapi waliokamatwa kwa uhujumu uchumi?
Ni jambo linalosikitisha na kuhuzunisha kuona , Serikali ikiwa makini kukusanya kodi kutoka kwa wafanyakazi nchini na kuziacha  Sh300 bilioni zilizopotea kwa mwaka mmoja  kutokana na wahujumu uchumi ambao hawajakamatwa hata mmoja.
 Je fedha hizo, kwa hali ya kawaida zisingetosha kuwaongezea mshahara wafanyakazi walau kwa Sh5,000 tu.
Kwa mawazo ya kawaida, kitendo cha serikali  kukaa kimya ama kuweka kwenye kumbukumbu za maandishi kukiri kwamba Sh300 bilioni zimepote kutokana na uchakachuaji bila ya hatua zozote zilizochukuliwa kwa wahusika  kinaonyesha kwamba serikali yenyewe inahusika.
Ni vigumu kuamini kwa jinsi  Mamlaka ya Kodi nchini (Tra) inavyohangaika kusaka fedha kutoka kwa walipa kodi wachache, lakini wasifuatilie  na kuyataja majina ya wachakachuaji, wa mafuta hadharani.

Lakini pia   kwa jinsi serikali inavyotunza kumbukum bu za madeni kwa waliopoteza fedha za umma ama kutumia vibaya  ni vigumu kuamini  sababu za kujua takwimu bila ya kuwatia ndani wahusika.

Bila Shaka Dk Balele alirudia kutaja takwimu za hasara kwa taifa ya Sh300 bilioni huku akiuma kidole kwamba kama angepewa nafasi ya kuwasaka angeanzia na wenye magari 18 ya Tanzania ambayo yalikutwa na mafuta yaliyochakachuliwa nchini Rwanda.

Hivi karibuni tumeshuhudia magari takribani 18 yakirejeshwa kutoka nchini Rwanda kwa sababu yalibainika kubeba petroli iliyochakachuliwa kutoka Tanzania.
Je wenye madereva, wenye magari, wamechukuliwa hatua gani? , Ni kweli Serikali inaona tukio hilo kuwa ni dogo?
Ki msingi kwa matukio makubwa ya kifisadi yanayogunduliwa na kutangazwa na vyombo mbalimbali duniani, hayana budi pia majibu yake  ama hatrua zinazochukuliwa kutangazwa hadharani ili kuzima moto.

Ni fedheha kwa serikali kuvielekeza vyomboi vingine vichukue hatua wakati  watu wanaliangamiza Taifa.
Pamoja na kazi nyingi nzuri za serikali iliyopo madarakani zilizotekelezwa kwa maendeleo, ipo haja ya kushughulikia waziwazi wezi au waharibifu wa uchumi wa Taifa.

Serikali ikikaa kimpya dhidi ya wachakachuaji na wezi wa fedha za miradi  kwa ujumla  kutawafanya Watanzania wawe na imani kwamba wahusika wakuu ni vigogo wa serikali yenyewe.
0767-338897


Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner