
| Ujamaa uliziunganisha Tanganyika na Zanzibar | Send to a friend |
| Friday, 09 December 2011 11:56 |
|
Fidelis ButaheJAMHURI ya Muungano wa Tanzania iliundwa Mkataba wa Muungano ulitiwa saini na aliyekuwa rais wa Tanganyika, Mwalimu Julius Nyerere na aliyekuwa rais wa Zanzibar, Sheikh Abeid Amani Karume, Aprili 22, 1964 huko Zanzibar. Mkataba huo ulithibitishwa na Bunge la Tanganyika na Baraza la Mapinduzi, Aprili 26 hadi 27, 1964. Jina la “Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar” lilibadilishwa Oktoba 28, 1964 na kuwa Ilivyokuwa Vyanzo mbalimbali vya habari vinaeleza kuwa Watanganyika kama ilivyokuwa kwa wananchi wa nchi nyingine za kiafrika, hawakukubaliana na utawala wa kikoloni. Tangu mwanzo waliwapinga huku upinzani mkubwa ukionyeshwa na kabila la Wasambaa wakiongozwa na Kimweri dhidi ya Wajerumani. Wahehe wakiongozwa na Mkwawa kupigana Kukosekana kwa umoja kati ya wapigania uhuru wa mwanzo na uimara wa majeshi ya wakoloni yaliyokuwa na silaha bora za moto, kulidhoofisha mapambano ya uhuru na kusababisha hasara kubwa na kupoteza maisha ya watu. Kama ilivyokuwa kwenye makoloni mengi ya kiafrika, hisia za utaifa ziliendelea kuimarika katika Tanganyika baada ya mwaka 1945. Alama za utaifa zilianza kuonekana mara baada ya vita kuu ya kwanza ya dunia, kwa kuanzishwa kwa vyama mbalimbali vya Waafrika kwa upande wa Tanganyika na Zanzibar. Kwa upande wa Tanganyika, African Association kilianzishwa mwaka 1929 kama kikundi cha mijadala baina ya wasomi na ilipofika mwaka 1948 chama hiki kikawa Tanganyika African Association (TAA). Baada ya vita ya pili ya Dunia, wanachama wa Tanganyika African Association (TAA) waliendeleza wimbi la utaifa. Mwaka 1953 chini ya uongozi wa Mwalimu Nyerere, TAA ilitambuliwa kama chama cha siasa na kuelekea moja kwa moja kuanzishwa kwa TANU mwaka 1954, chama kilichotumika kama chombo cha kisiasa cha watu katika kutoa vilio vyao vya kudai uhuru. Kuanzishwa kwa TANU mwaka 1954, ulikuwa ndio Baada ya miaka saba ya mapambano ya kisiasa, Tanganyika ilikuwa huru chini ya chama cha
Kwa upande wa Zanzibar, chimbuko la Jumuiya ya Waafrika ilikuwa ni vilabu vya mpira wa miguu vilivyoanzishwa mwanzoni mwa miaka Ilipofika mwaka 1934, Jumuiya ya Waafrika ilianzishwa rasmi na kupewa jina la African Association (AA). Baada ya vita ya pili ya dunia kama ilivyokuwa katika sehemu nyingine za dunia, kulikumbwa na uhaba mkubwa wa chakula, ubaguzi na mgawanyiko baina ya jamii. Kutokana na matatizo hayo ya ubaguzi, kulianzishwa
Waligundua kuwa Serikali ya kikoloni na chama cha ZNP walishirikiana kuendeleza dhuluma dhidi ya Waafrika. Viongozi hao waliona ulazima wa kuungana kuwa kitu kimoja kupigania uhuru. Katika kutekeleza azma hiyo, viongozi wa Jumuiya hizo walikutana na kukubaliana kuunganisha Shirazi Association na African Association mwaka 1957. Muunganiko huo ulisababisha kuundwa kwa chama cha Afro- Shirazi Union ambacho baadae kiliitwa Chama cha Afro-Shirazi chini ya uongozi wa Sheikh Abeid Amani Karume. Vuguvugu la kisiasa Kati ya mwaka 1957, mara baada ya uchaguzi mkuu wa kwanza na mwishoni mwa mwaka 1963, kabla ya mapinduzi ya mwaka 1964, Zanzibar ilitawaliwa na vuguvugu na mivutano mikali ya kisiasa.
Chama cha ZNP baada ya kushindwa uchaguzi, kilianzisha kampeni za kushawishi wenye mashamba na mabepari wengine waliokuwa wakimiliki njia kuu za uchumi kuwafukuza kazi au kutowaajiri wafuasi wa ASP. Chama cha ZNP kiliwatafutia kazi na kuwabakisha mashambani waafrika wote waliokubali kukiunga mkono. Wakati wa mvutano huo wa kisiasa kati ya ASP na ZNP ukipamba moto, kulijitokeza tofauti miongoni mwa viongozi wa ASP.
Migogoro hiyo ilisababisha kujitoa kwa baadhi ya viongozi wa ASP ambao walifanya mkutano na baadhi ya wanasiasa mashuhuri wa ASP huko Pemba, Novemba 1959 na walikubaliana kuanzisha Chama kipya cha siasa cha Zanzibar and Pemba People’s Party (ZPPP). Uchaguzi ulifanyika Januari 16, 1961 ambapo siku moja kabla ya uchaguzi huo, serikali ilitangaza kuwa chama kitakachoshinda kitaunda serikali na wizara zote zitakuwa chini yake. Katika uchaguzi huo ASP ilishinda kwa kupata Kutokana na kuenea kwa chuki za kisiasa miongoni mwa Wazanzibari, Vyama vikuu vya kisiasa vilifikia muafaka wa kumaliza hali hiyo. Hatahivyo, ASP haikufikisha zaidi ya nusu ya kura na hivyo haikuweza kuunda serikali. Njia pekee iliyobakia ilikuwa ni kuishauri ZPPP ZPPP na ZNP viliungana na iliamuliwa kuwa iundwe serikali ya muda na kusubiri uchaguzi mwingine uliopangwa kufanyika Juni, 1961.
Chini ya ushauri wa Waingereza, Shamte aliwatenga ndani ya Serikali yake baadhi ya viongozi wa ZNP wenye msimamo wa Kikomunisti wakiongozwa na Abdulrahaman Babu, na hivyo kutokea kutofautiana kwa baadhi ya viongozi wa ZNP na Serikali ya ZNP/ZPPP.
Makubaliano ya Waingereza na Wajerumani ya mwaka 1890 yalifanya Zanzibar kuwa koloni la waingereza ambao walimshirikisha Sultani katika utawala wao.
Waingereza walifanya Zanzibar kuwa ni koloni la Waarabu na ilipofika Desemba 1963, Sultani alipewa mamlaka kamili ya kutawala Zanzibar. Januari 12, 1964, aliyekuwa Sultani wa Zanzibar, Jamshid bin Abdulla, aling’olewa madarakani katika mapinduzi yaliyokuwa yameandaliwa kwa usiri, ustadi na ujasiri mkubwa wa wanamapinduzi wa ASP na Jamhuri ikatangazwa. Muungano Muundo wa muungano wa Tanganyika na Zanzibar uliozaa nchi ya Tanzania kama ulivyoelezwa katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, una vyombo viwili vyenye mamlaka ya utendaji ambavyo ni Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Pia kuna vyombo viwili vyenye mamlaka ya kutunga sheria na kusimamia utekelezaji wa shughuli za umma ambavyo ni Bunge na Baraza la Wawakilishi. Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ni ushahidi unaojitosheleza kuwa wananchi
Sababu za muungano huo ni pamoja na kuwepo kwa mahusiano ya karibu ya kihistoria baina ya Moyo wa kuwa na muungano wa Afrika kwa kuanzia na Shirikisho la Afrika Mashariki ulianza hata kabla ya uhuru wa Tanganyika. Mwalimu Nyerere pamoja na viongozi wengine waliokuwa wakipigania utaifa katika ukanda wa Afrika Mashariki walikuwa na matarajio ya kuwa na Muungano wa Afrika.
Baada ya kushauriana na viongozi mbalimbali wa iliyokuwa Jumuiya ya Wapigania Uhuru wa Afrika Mashariki na Kati (Pan- African Freedom Movement for East and Central Africa - PAFMECA) Mwalimu Nyerere alitoa tamko wakati wa mkutano wa nchi huru za Afrika uliofanyika Addis Ababa mwaka 1960. Katika mkutano huo Nyerere alizungumza mambo mengi na baadhi yalinukuliwa katika gazeti la Tanganyika Standard, Novemba 1964). Alisema, ““Wengi wetu tunakubaliana bila kikwazo kwamba Shirikisho la Afrika Mashariki litakuwa ni jambo zuri. Tumesema na ni kweli kwamba mipaka inayotenganisha nchi zetu imewekwa na
|















Comments